Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wizara Ya Kilimo

TAASISI YA UTAFITI WA KILIMO TANZANIA

Adoption and Impact studies

Ufuatiliaji wa Upitishaji na Athari za Teknolojia

Kitengo cha Uchumi wa Jamii hushughulikia tafiti za upokelewaji wa teknolojia (adoption) na athari (impact) za aina mbalimbali za mazao na teknolojia za kilimo. Tafiti hizi huchambua jinsi wakulima na wadau wengine wanavyotumia teknolojia mpya za kilimo na sababu zinazochangia au kuzuia matumizi yake.

Pia, tafiti hizi hupima athari za kiuchumi, kijamii, na kimazingira za teknolojia hizo, na kutoa mrejesho (feedback) wa kuboresha utafiti, kusaidia katika utungaji wa sera, na kuwezesha maamuzi sahihi ya uwekezaji katika sekta ya kilimo.