Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wizara Ya Kilimo

TAASISI YA UTAFITI WA KILIMO TANZANIA

Tunafanya Nini

Utafiti na Ubunifu

Uendelezaji wa teknolojia na ubunifu unafanywa chini ya mada mbalimbali: Uboreshaji wa mazao, Agronomia, Ulinzi wa mazao, Usimamizi baada ya mavuno, Uchumi wa kijamii, Jinsia na Masoko, Usimamizi wa rasilimali za asili, Utoaji wa mashine za kilimo, na Uhandisi wa kilimo.

Uhifadhi wa Mbegu

Kuzalisha mbegu za kizazi cha awali (pre-basic na basic seed) na mbegu zilizothibitishwa (certified seed) za aina za mazao yaliyoboreshwa kwa wadau wengine katika mnyororo wa thamani ya mbegu. Aidha, TARI inahifadhi mbegu za aina mbalimbali za mazao ili kuhakikisha ubora na usafi wake.

Cheti cha Idhini ya Maadili 

Hutoa idhini na kusimamia masuala ya maadili kwa taasisi za kimataifa na za ndani pamoja na watu binafsi wanaofanya utafiti wa kilimo katika Tanzania Bara.

Usajili wa Utafiti wa Kilimo

Usajili wa taasisi na watu binafsi wanaofanya shughuli au miradi ya utafiti wa kilimo katika Tanzania Bara.

Mafunzo

TARI hufanya mafunzo mbalimbali kwa wadau tofauti wa kilimo ili kuboresha usalama wa chakula, lishe, na kipato, pamoja na kupunguza kazi ngumu. Mafunzo haya kwa kawaida ni juu ya:

  • Mbinu Bora za Kilimo 

  • Usimamizi baada ya mavuno

  • Kuongeza thamani 

  • Uchumi wa kijamii

  • Kuingiza masuala ya jinsia 

Huduma za Maabara

Kufanya uchambuzi wa sampuli za udongo na mimea ili kubaini virutubisho, utambuzi na uchunguzi wa wadudu na magonjwa, na DNA fingerprinting.

Ushauri 

Huduma za kiufundi na ushauri kwa watu binafsi na taasisi.

Takwimu 

Ukusanyaji, upangaji, na uchambuzi wa data za utafiti wa kilimo.