Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wizara Ya Kilimo

TAASISI YA UTAFITI WA KILIMO TANZANIA

Karibu

Karibu katika tovuti ya Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI), kitovu cha Taifa cha ubunifu wa kilimo, ubora wa utafiti, na suluhisho endelevu kwa wakulima.

TARI tunaamini kuwa kilimo ndicho uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania na ufunguo wa kufikia usalama wa chakula, uhifadhi wa mazingira, na ukuaji jumuishi wa kiuchumi. Timu yetu yenye watafiti, wanasayansi, wahandisi na watumishi wenye kujituma inafanya kazi kwa bidii kote nchini ili kuendeleza na kusambaza teknolojia na mbinu bunifu zinazowawezesha wakulima na kubadilisha maisha ya wakulima kuelekea uchumi bora na maisha bora.

Tukiwa na msingi imara wa kisayansi na dhamira thabiti ya kutoa huduma, tunajivunia kuongoza katika sekta ya utafiti na maendeleo ya kilimo. Iwe wewe ni mkulima, mtunga sera, mshirika wa maendeleo au mtafiti, tunakukaribisha kusoma na kufuatilia kazi zetu, kuwasiliana na wataalamu wetu, na kuungana nasi katika kujenga sekta ya kilimo yenye tija na ustahimilivu zaidi kwa Tanzania na kwingineko.

Pamoja, tukuze ubunifu wa kilimo kwa ajili ya kesho iliyo bora zaidi.